Breaking News

Ijumaa, 6 Novemba 2015

Ungana nasi katika uapisho wa Rais Magufuli

1.12pm:Sasa rais Magufuli akiandamana na mkewe wanaondoka katika uwanja wa Uhuru baada ya kuapishwa rasmi.
1.09pm:Amewataka viongozi wa upinzani kushirikiana na serikali yake akisisitiza kuwa uchaguzi umekwisha na kwamba rais aliyechaguliwa ni John Pombe Magufuli

  Rais wa Serikali ya awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Joseph Magufuli akiwa na Makamu wake Mama Samia Suluu,baada ya kuapishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania 
1.06pm:Magufulu aipongeza tume ya uchaguzi kwa kufanya uchaguzi ulio huru mbali na vyombo vya usalama vilivyoimarisha amani.Awashukuru wanahabari kwa kuwaelimisha raia wa Tanzania
1.05pm:'Sasa ni kazi tu' awataka viongozi wa upinzani kushirikiana kwa lengo la kuendeleza na kuwahudumia watanzania
1.04pm:''Nashukuru wagombea wanzangu kwa kutupa chanagmoto,tumejifunza mengi kutoka kwao''.
1.03pm:''Natambua kwamba nina jukumu kubwa la kuwafanyia kazi watanzania,lakini hatahivyo tumuweke mungu mbele ili kutekeleza ahadi hizo.
1.02pm:Magufuli:Nawashkuru watanzania kwa kunichagua kwa kura nyingi ili kuongoza taifa kwa miaka mitano ijayo.
1.01apm:Magufuli:Nawashukuru viongozi mbali,mbali waliowasili hapa ili kujumuika nami katika sherehe hii muhimu.
1.00pm:Namshkuru sana mwenyezi mungu aliyetujalia kuwepo hapa pamoja na viongozi wa dini.
12.58pm:Na sasa ni wakati wa rais John Pombe Magufuli kulihutubia taifa.

 Viongozi watambulishwa kwa umati,Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe,wapili kulia,Rais wa Rwanda Paul Kagame kushoto,Rais wa DR Congo Raurent Kabila kulia,Rais wa Kenya Uhuru Kenyata wa tatu kulia.
12.06am:Marais na viongozi mbalimbali waliowasili katika hafla hiyo watambulishwa kwa wananchi waliojaa katika uwanja huo.

Rais Magufuli akipigiwa mizinga 21, kama ishara ya kukaribishwa katika utawala mpya wa nchi.
12.00am:Na sasa kamanda wa jeshi anaomba rukhsa ya kuondoka uwanjani.

Rais wa awamu ya tano John Pombe Magufuli kulia, akiwa na rais wa awamu ya nne Jakaya Kikwete, wakipokea salamu za utii kutoka kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Genali Davis Mmwamunyange kulia na mlinzi wa rais kushoto.
11.56am:Ndege za kijeshi zinapita juu ya uwanja wa Uhuru kutoa heshima kwa rais mpya wa taifa hilo John Pombe Magufuli.
11.27am:Rais Magufuli alikagua gwaride la heshima
11.23am:Mizinga 21 ya kumkaribisha rais mpya wa Tanzania John Pombe Magufuli yapigwa
11.22am:Jeshi laomba rukhsa kutoka kwa rais mpya wa Taifa la Tanzania John Pombe Magufuli

                                                             Jukwaa la kula kiapo
11.20am:Jakaya Mrisho Kikwete sasa awasalimia viongozi waliofika katika jukwaa la waheshimiwa wakiwemo marais mbalimbali.

Rais aliyemaliza muda wake,Jakaya Mrisho Kikwete,kushoto akiwa na aliyekuwa makamu wake Dk Mohamed Garrib Bilal,wakiondoka Uwanjani kwa gari la wazi kama ishara ya kuachia madaraka kwa serikali mpya.
11.18am:Sasa jeshi lamuaga aliyekuwa rais wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete na aliyekuwa makamu wake Gharib Bilal
10.55am:Makamu wa rais wa Kwanza mwanamke nchini Tanzania Samia Suluhu Hassan aapishwa

Rais Dk John Pombe Joseph Magufuli,akionyesha slaa za jadi za asili ya mtanzania kama ishara ya kuwa Amiri Jeshi Mkuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wa Tanzania
10.51am:Rais mpya wa Tanzania apewa mkuki na ngao ya ishara ya kuchukua madaraka.
10.48am:''Mimi John Pombe Magufuli naapa nitatenda kazi zangu za urais kwa mujibu wa sheria na mila na desturi za muungano wa Tanzania,ewe mwenyezi mungu nisaidie''
10.47am:Rais mteule John Pombe Magufuli aapisshwa .Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya pia amewasili hapa.

      Bendera ya Rais Kikwete ikishushwa kuashiria mwisho wa utawala wake.
10.45am:Na sasa aliyekuwa rais wa taifa hilo Jakaya Kikwete amekuwa raia wa kawaida baada ya bendera ya utawala wake kushushwa hapa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam
10.40am:Wimbo wa Taifa la Tanzania wapigwa na baadaye bendera ya rais Kikwete itashushwa ili kuashiria mwisho wa uoingozi wake.

              Rais Jakaya Kikwete,akipigiwa mizinga 21 ya mwisho katika utawala wake
Mizinga 21 ya kutoa heshima za mwisho kwa rais Jakaya Kikwete yapigwa.

                                             Kikwete akizunguka uwanja
10.21am:Gari la gwaride la kijeshi lililombeba rais Kikwete sasa lauzunguka uwanja huo huku wananchi waliojjaawa na furaha wakimsalimia kwa kumpungia mkono.
10.20am:Na sasa msafara wa Rais Jakaya Kikwete wawasili katika uwanja wa Uhuru .KIkwete baadaye anaonekana kuingia katika gari rasmi la gwaride katika uwanja wa uhuru na kuwapungia mkono maelfu ya wananchi waliojaa katika uwanja huo.
10.15am:Rais Mteule John Pombe Magufuli awasili katika sherehe hizo na kulakiwa na jaji mkuu Othman Chande.

                                                              Uwanja wa Uhuru
9.48am:Rais wa Rwanda Paul Kagame anawasili katika uwanja wa uhuru na kuketi bega kwa bega na waliokuwa marais wa taifa hilo Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa.
9.47am:Rais wa kisiwa cha Zanzibar Dokta Ali Mohammed Shein amewasili katika uwanja wa Uhuru na anaonekana hapa akisalimiana na rais mstaafu wa Tanzania Hassan Mwinyi.Kumbuka kiongozi huyo wa Zanzibar aliongezewa mda wa kuhudumu katika kisiwa hicho baada ya tume ya uchaguzi kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa urais katika kisiwa hicho.
9.43am:Rais mteule John Pombe Magufuli atakuwa rais wa awamu ya tano kuchaguliwa nchini Tanzania tangu taifa hilo lijipatie Uhuru.

                                                      Raia waliowasili uwanjani
9.39am:Vilevile aliyekuwa waziri mkuu nchini Kenya Raila Odinga ambaye ni rafiki mkubwa wa rais mteule John Pombe Magufuli,rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph kabila pamoja na rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ni baadhi ya viongozi waliowasiliili kuhudhuria sherehe hiyo ya kihistoria.
9.35am:Miongoni mwa viongozi wanaotarajiwa katika hafla hii ni pamoja na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ambaye tayari ameondoka katika uwanja wa Jomo Kenyatta Jijini Nairobi akiandamana na Mkewe bi. Margeret Kenyatta na anatarajiwa kuwasili katika uwanja wa sherehe hizi wakati wowote kutoka sasa
9.30am:Gwaride la kijeshi tayari limejiandaa vilivyo ikiwemo wanajeshi waliovalia sare za rangi tofauti hapa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

                                                                     Mapambo
8:00 am Mataifa mbalimbali yamekuwa yakituma risala za pongezi kwa Tanzania na kwa Rais Mteule John Magufuli.
Wa kwanza kutuma risala za pongezi walikuwa ni:
Rais wa Rwanda Paul Kagame na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kiarabu ya Saharawi Mohammed Abdelaziz.
Katika salamu zake kwa Rais Mteule Magufuli, Bw Kagame amesema: "Kufuatia kuchaguliwa kwako kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, napenda kukutumia Mheshimiwa salamu za dhati, pongezi na heri nyingi kwa niaba yangu mwenyewe, Serikali yangu na wananchi wa Rwanda.”
Naye Rais Abdelaziz amemwambia Rais Mteule Magufuli: “Sisi tuna uhakika kuwa chini ya uongozi wako wa busara, Tanzania itaendelea kusonga mbele na kupata maendeleo na ustawi mkubwa zaidi.”
7:10 am Viongozi wa baadhi ya mataifa ya Afrika wanatarajiwa kuhudhuria wakiwemo Jacob Zuma kutoka Afrika Kusini, Robert Mugabe kutoka Zimbabwe na Filipe Nyusi wa Msumbiji. Mhubiri mashuhuri kutoka Tanzania TB Joshua pia atahudhuria sherehe hiyo.
7:00 am Watumbuizaji wanaotarajiwa kutumbuiza wakati wa sherehe walifika uwanjani mapema na ala zao.

6:45 am Uwanja umeanza kujaa watu. Wengi wa waliofika mapema wanafurahisha kujipiga, kupigana na kupigwa pichwa kuweka kama kumbukumbu za siku hii.

Image caption Baadhi ya waliofika wamevalia mavazi yenye rangi za chama tawala CCM

6:30 am Uwanja wa Uhuru umepambwa ukapambika

                                                 Uwanja wa Uhuru

6:30 am Waandishi wa BBC wamo katika uwanja huo kukuletea habari kadiri zinavyochipuka.

Mubali
                                       Mwandishi wa BBC Leonard Mubali

6:30 am Sherehe ya kumuapisha Bw Magufuli inafanyika katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

                       Usalama umeimarishwa katika uwanja huo
6:00 am. HABARI YA ASUBUHI?
Rais Mteule wa Tanzania John Pombe Magufuli anaapishwa leo kuwa rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kutangazwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Oktoba 25.
Rais Magufuli alipata asilimia 58.46 ya kura zilizopigwa kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania. chanzo BBC/Swahili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni