Breaking News

Jumapili, 15 Novemba 2015

Tujikumbushe uzembe wa mabeki wa Stars

Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars jana ilishindwa kutumia uwanja wake wa nyumbani baada ya kulazimishwa sare ya mbao 2-2 dhiti ya Algeria kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Tanzania ambayo ilianza kusaka ushindi kwa nguvu zote ilishindwa kutumia nafasi za wazi zaidi ya 15 baada ya washambuliaji wake Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu ,Elias Maguli kukosa umakini katika lango la wapinzani.

Hata hivyo goli la dk 40 lilofungwa na maguli na dk 60 iliyofungwa na Samatta ilitosha kuifanya timu hiyo kutawala mpira, kabla ya makosa ya mabeki kuruhusu magoli 2 ndani ya dk 5, na kuifanya Algeria kusawazisha mabao yote na kubali ubao wa matangazo kuwa 2-2.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni