Breaking News

Jumanne, 8 Desemba 2015

Magufuli aongoza Watanzania kufanya usafi

Magufuli aongoza Watanzania kufanya usafi  


Magufuli
Image captionRais John Magufuli ameagiza siku ya Uhuru itumiwe kufanya usafi

Raia nchini Tanzania wameungana na maafisa wa serikali kuitikia wito wa Rais John Magufuli wa kutumia Siku ya Uhuru kufanya usafi.
Mamia ya watu walirauka na kuanza kusafisha baadhi ya maeneo ambayo hujulikana sana kwa kuwa na uchafu na taka kwa wingi.
Mwandishi wa BBC Sammy Awami aliwapata wachuuzi na maafisa wa baraza la jiji Dar es Salaam asubuhi na mapema wakifanya usafi katika soko maarufu la Kariakoo.

Usafi
Image captionMaafisa wa serikali wanasaidiana na raia

Wengi wamefurahia agizo la Rais.
Mwandishi wa BBC Tulanana Bohela anasema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pia amefika soko hilo la Kariakoo.
Rais John Magufuli naye amekuwa kwenye aneo la ufuo wa bahari karibu na ikulu akiwa amevalia glavu.
Katika eneo la Mwenge, wananchi pia wanajizatiti kufanya usafi. Mwandishi wa BBC Regina Mziwanda amewapata wananchi hawa wakiteketeza takataka baada ya kuzikusanya pamoja.

Taka
Image captionWakazi wakichoma taka eneo la Mwenge

Hata katika maeneo ya kifahari, wananchi wamejitokeza kufanya usafi.

US presidential candidate Ben Carson to visit Kenya


By KEVIN J. KELLEY
More by this Author

NEW YORK
A Republican Party candidate for the US presidency said on Monday he plans to visit Kenya later this month.
Dr Ben Carson, a retired neurosurgeon, cited his East African ancestry as a key reason for the trip.
"My ancestors are from the Kenya-Tanzania region, the Turkana tribe. I’ve had all of that traced back," Dr Carson told a US radio talk-show host.
The 64-year-old candidate has seen his once strong support slip in recent polls of Republican voters from 22 per cent in October to 14 per cent in a survey released last week.
The rating places Dr Carson third among the 13 politicians seeking the 2016 Republican presidential nomination.
He trails businessman Donald Trump, who registered 36 per cent in the same poll, and Senator Ted Cruz, whose support stood at 16 per cent.
Dr Carson acknowledged on Monday that his lack of international policy experience may account for his drop in the voter survey.
His planned trip to Africa, which includes stops in Nigeria and Zambia, is seen as part of an effort to assuage doubts about his ability to lead the US on the world stage.
BOKO HARAM
Dr Carson has made erroneous comments on some key foreign policy issues, suggesting, for example, that China is militarily involved in Syria.
In a speech to a US Jewish group last week, he mispronounced the name of the Palestinian militant group Hamas, calling it "hummus".
His claim that the Turkana people occupy "the Kenya-Tanzania region" appears to be another instance of confusion on Dr Carson's part.
The Turkana live in northwest Kenya near the borders with South Sudan, Ethiopia and Uganda –an area far from Tanzania.
Dr Carson said on Monday that in Nigeria, he intends to assess the nation's economy and the threat it faces from Boko Haram.
"Also, there’s a medical school there named after me which I want to visit," he added.
Dr Carson said he will visit Zambia, which is the homeland of conjoined twins, Joseph and Luka Banda, whom he and his team of surgeons successfully separated in 1997.
"They were joined at the top of the head facing in opposite directions almost 18 years ago and this is the year they graduate from high school,” he said.
He is scheduled to travel to Africa on December 27 and return to the US a week later. Source Daily Nation 

Magufuli ateka kampeni za urais Uganda

Kasi ya Rais John Magufuli katika kubana matumizi yasiyo ya lazima ya serikali ili fedha zinazookolewa zielekezwe katika kuimarisha huduma za jamii imeendelea kuvutia wengi katika nchi jirani za Afrika Mashariki.
Kasi ya Rais John Magufuli katika kubana matumizi yasiyo ya lazima ya serikali ili fedha zinazookolewa zielekezwe katika kuimarisha huduma za jamii imeendelea kuvutia wengi katika nchi jirani za Afrika Mashariki baada ya jina lake kuanza kutumiwa na wagombea urais nchini Uganda.
Kati ya wagombea wote, aliyejipambanua kwa uwazi kuwa atafuata nyayo za Magufuli katika kuhakikisha kuwa serikali inaendesha mambo yake kwa nia ya kubana matumizi yasiyo ya lazima, kukomesha ufisadi na mwishowe kuwanufaisha watu wa tabaka la chini kupitia uboreshaji wa huduma za jamii ni mgombea wa upinzani anayemtikisa Rais Yoweri Museveni katika kinyang’anyiro hicho, Dk. Kizza Besigye wa chama cha Forum for Democratic Change (FDC).
Katika kampeni zake mwishoni mwa wiki, Besigye amesema wazi kuwa pindi atakapochaguliwa na wananchi na kuingia madarakani, atafuata nyayo za Magufuli kwa kuanza kuipiga bei ndege inayotumiwa na Museveni kwa maelezo kuwa inalibebesha taifa lao gharama kubwa ambazo zinaweza kutumiwa katika kuboresha huduma za jamii.
Besigye alisema yeye anaunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais mpya wa Tanzania, Magufuli, ambaye anaishi kulingana na jina lake la utani la ‘tingatinga’ kutokana na kuchukua hatua kadhaa dhidi ya ufisadi, kuongeza ufanisi wa kazi katika ofisi za umma na pia kuongeza nidhamu ya matumizi kwa manufaa ya taifa na siyo watu wachache.http://www.eatv.tv/news/current-affairs/magufuli-ateka-kampeni-za-urais-uganda

Kaburi la halaiki lapatikana Kenya

Image captionKaburi la halaiki lapatikana Kenya
Wakaazi wa mji wa Mandera, kaskazini mashariki mwa Kenya wanasema wamegundua zaidi ya miili 20 iliyozikwa kwenye makaburi ya jumla.
Miongoni mwa miili hiyo ni ule wa mama mmoja aliyeripotiwa kupotea siku tano zilizopita.
Picha za kusikitisha zilisambaa mitandaonii asubuhi ya leo, zikionyesha sehemu za mwili za watu zikichomoza kutoka makaburi yaliyochimbwa juu juu.
Miili mingine ilikuwa uchi. Mwili wa mama ulioonekana kuharibiwa ulizua hisia nzito zaidi.
Marehemu asemekana alikuwa mama wawatoto watano, aliyekamatwa na watu wasiojulikana siku nne zilizopita.
Seneta wa eneo hilo Billow Kerrow alieleza ugunduzi huo kama wa kutisha, na kudai waliouwawa ni waathirika wa mauaji ya serikali.
Image captionInspekta mkuu polisi Joseph Boinnet alidhibitisha kifo cha mwanamke huyo, lakini akakanusha madai kuwa kuna makaburi ya jumla.
Inspekta mkuu polisi Joseph Boinnet alidhibitisha kifo cha mwanamke huyo, lakini akakanusha madai kuwa kuna makaburi ya jumla.
Makundi ya kutetea haki za kibinadamu yanaamini kuwa askari wa kupambana na ugaidi kwa kawaida kuwaua washukiwa.
Aidha wamekashifu vyombo vya usalama kwa kupuuza taratibu za kisheria na kuwaua mashahidi kabla ya kesi zao kumalizika.
Serikali imewahi kuitaja mahakama kama bodi inayovunja guu vita dhidi ya ugaidi.
Mwaka jana Makamu wa Rais William Ruto alisema washukiwa wa ugaidi huachiliwa kwa dhamana kwa urahisi sana wanapofikishwa mahakamani , kisha wao hutoweka wasionekane tena.
Mnamo Mwezi mwei, miili kumi na moja ilipatikana kwenye makaburi mjini wajiri, kusini mwa Mandera.
Mabaki ya risasi yaliyopatikana kando ya makaburi hayo yalizua shauku zaidi kuwa huenda polisi wa kupambana na ugaidi walihusika.

Mwezi mmoja wa uongozi wa Magufuli Tanzania

Ni siku thelathini tu tangu rais mpya wa Tanzania John Pombe Magufuli aingie madarakani, lakini kasi ya utendaji wake umeibua hisia mbalimbali nchini humo, nchi za jirani na hata zingine za mbali barani Afrika.

Kuanzia kuwasimamisha kazi maofisa waandamizi wa serikali na mashirika ya umma hadi kufuta kwa sherehe za maadhimisho kadhaa utendaji wake umetia shauku ya watu kutaka kujua uongozi wake utaleta chachu gani nchini Tanzania.
Mwandishi wa BBC Sammy Awami amedodosa hilo zaidi.

Jumatatu, 7 Desemba 2015

Mbona Wakenya wanamkaribisha Kenyatta kama mgeni?

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amefanya ziara 43 nje ya nchi tangu kuingia madarakani miaka mitatu iliyopita na Alhamisi wiki hii anatarajiwa kuzuru Kigali, Rwanda.
Ziara hizi zimeonekana kuwakera wananchi wengi ambao wameingia kwenye mitandao ya kijamii kuzikosoa.
Kwa takriban siku mbili, jumbe za kukejeli safari hizo zimekuwa mada kuu katika mitandao ya kijamii, Wakenya wakitumia kitambulisha mada #UhuruInKenya.
Wanalinganisha kurejea kwa Rais Kenyatta nchini Kenya kutoka Afrika Kusini na ziara zilizofanywa na viongozi mashuhuri duniani kama vile Rais Barack Obama mwezi Julai na Papa Francis mwezi Novemba. Vitambulisha mada vilivyotumiwa wakati huo vilikuwa #ObamaInKenya na #PopeInKenya.
Bw Kenyatta amefanya ziara 43 katika muda ambao amekuwa uongozini, ambazo zinazidi ziara 33 za nje ya nchi alizofanya mtangulizi wake Rais mstaafu Mwai Kibaki miaka kumi aliyokuwa mamlakani.
Ziara hizo za Rais Kenyatta zinakadiriwa kugharimu Sh2.1 bilioni, kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation.
Lakini ikulu imetetea ziara hizo ikisema zimeletea Kenya manufaa tele.
Msemaji wa Rais Manoah Esipisu alihutubia wanahabari Jumapili na kusema Bw Kenyatta amefanikiwa kupata ufadhili wa miradi ya miundo mbinu, elimu, kawi na masoko ya bidhaa.
Kunao wanaoamini ziara hizo zinastahiki, kwa mfano mdadisi wa masuala ya kisiasa Mutahi Ngunyi anayesema Bw Kenyatta anafaa kuachwa afanye kazi.
Baadhi ya Wakenya wamelinganisha mtindo wa Bw Kenyatta na kiongozi wa taifa jirani la Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ambaye kwa mwezi mmoja ambao amekuwa madarakani ameonekana kutilia mkazo sana kupunguzwa kwa matumizi ya fedha za umma.
Amefuta ziara nyingi za ng'ambo na kuwapa mabalozi wa taifa hilo nchi za kigeni jukumu la kuwakilisha taifa.
Dkt Magufuli ametumia kauli mbiu ya "Hapa Kazi Tu" wakayi wa kampeni na baada ya kuingia uongozini. Kauli mbiu hii imefanyiwa ukarabati na baadhi ya watu na kugeuzwa kuwa "Hepa Kazi" upande wa kiongozi wa Kenya.

Magufuli avunja bodi ya bandari Tanzania

Rais wa Tanzania John Magufuli amevunja bodi simamizi ya bandari siku chache baada ya kupatikana kwa makontena ambayo hayakuwa yamelipiwa ushuru bandari ya Dar es Salaam.
Tangazo la kuvunjwa kwa bodi hiyo limetolewa na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim kwenye kikao na wanahabari. Kampuni 43 ziligunduliwa kuhusika katika makontena hayo.
Prof Joseph Msambichaka ameondolewa kutoka kwa wadhifa wake kama mwenyekiti wa bodi ya bandari sawa na Bw Awadhi Massawe ambaye amekuwa akihudumu kama mkurugenzi mkuu.
Katibu mkuu wa wizara ya uchukuzi Dkt Shaban Mwinjaka pia ameondolewa wadhifani "kuanzia tarehe ya leo na atapangiwa kazi nyingine".
Bw Kassim alifanya ziara ya kushtukiwa wiki iliyopita katika bandari ya Dar es Salaam na ndipo akagundua makontena 329 yalipitishwa bila kulipiwa kodi kinyume na utaratibu wa bandarini.
Waziri huyo mkuu anasema ripoti ya ukaguzi wa ndani iliyotolewa Julai 30 mwaka huu ilionyesha makontena 2,387 yalipitishwa bandarini kinyume cha utaratibu kati ya Machi na Septemba 2014.
"Serikali haitavumilia kuona watu wachache au kikundi chochote kilichojipanga kuhujumu mifumo au kuiibia serikali kwa namna yoyote kwa manufaa ya wachache,” amesema Bw Majaliwa.
Miongoni mwa hatua alizochukua Bw Majaliwa ni kuagiza kubadilishwa kwa mfumo wa malipo hadi mfumo wa kielektroniki ambao unafaa kuwa umekamilika kufikia Ijumaa wiki hii.
Waziri mkuu huyo pia amewasimamisha kazi wasimamizi wanane wa Bandari Kavu.(Chanzo Bbc)