Breaking News

Jumamosi, 31 Oktoba 2015

Kagame ameanza kumchokonoa Magufuli

WAKATI RAIS mteule wa serikali ya awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Joseph Magufuli, akisubiri kuapishwa rasmi na kushika madaraka ya nchi, Rais wa Rwanda Poul Kagame ameibuka nakutangaza rasmi kwamba rais huyo si chaguo la watanzania.

Kagame alisema kwamba Rais Dk Magufuli ni chaguo la CCM na kwamba chama hicho kimeamua kuionyesha dunia kwamba hakuna demokrasia nchini Tanzania bali ni serikali ya kidikteta.

Kagame pia alisema kwamba Rais Magufuli atapata shida katika utawala wale kwa sababu anajua kwamba yeye si chaguo la wananchi. " The president Kagame of Rwanda says"Today may be the day that the president is sworn in,forcefully and in a draconian way;even when the majority voters disagree.Today CCM has decided to show the world that there is no democracy in Tanzania but a dictatorship government of CCM.T he president who will be sworn in will be a choice of CCM and not the majority voters.The president who will struggle to lead because he knows he was not peoples' choice but a shadow of previous presidents who have taken the control of election and force in power"

Ijumaa, 30 Oktoba 2015

Maoni ya mdau kupitia Facebook

Sina tatizo na ushindi wa urais wa Magufuli, ninachowalaumu wa Watanzania ni uamuzi wao wa kujaza wa Wabunge wengi wa CCM katika chombo muhimu cha uamuzi wa nchi hii.
Kitendo cha Watanzania kuwachangua zaidi wabunge 177 wa CCM ni wazi zile ndiyooo ambazo hazina tija zitaendelea kutawala zaidi na mambo mengi ya kitaifa yatakwama kwa sababu ya kosa hili.

Sioni jinsi mafisadi watakavyoweza kupelekwa katika mahakamani.
Lakini kwa sababu ujinga wetu tumeamua kumpa Magufuli wabunge wake wengi basi tujiandaa. Mungu ibariki Tanzania,  Andrew Kingamkono
Naamini Magufuli angefanya kazi kwa kasi zaidi kama angekuwa na idadi kubwa ya wabunge kutoka upinzani, lakini kwa hali ilivyo sasa, sioni jinsi Katiba ya wananchi itakavyoweza kurudishwa na kuheshimiwa, sioni jinsi mikataba mibovu ya madini itakavyojadiliwa kwa uwazi bungeni.

Magufuli apewa cheti cha ushindi Tanzania

Mgombea urais kupitia chama cha CCM John Mafuguli amepewa cheti cha ushindi baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili. Bw Magufuli amekabidhiwa cheti hiyo kwenye hafla iliyoandaliwa katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Hafla hiyo imehudhuriwa na kiongozi anayeondoka mamlakani Rais Jakaya Kikwete pamoja na waangalizi wa uchaguzi kutoka makundi mbalimbali.

                    Tume ya uchaguzi ilisema Magufuli alipata asilimia 58.46 ya kura zilizopigwa  

 Kadhalika, mgombea wa pekee mwanamke katika kinyang'anyiro hicho Bi Anna Mghwira wa chama cha ACT Wazalendo alihudhuria hafla hiyo, na kumpongeza Bw Magufuli kwa ushindi wake.
Kiongozi huyo mpya hakutoa tamko lolote wakati wa hafla hiyo na alifululiza moja kwa moja hadi ikulu chini ya ulinzi mkali.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania Jaji Mstaafu Damian Lubuva alisema Alhamisi kuwa Magufuli, alijipatia kura 8,882,935 ikiwa ni asilimia 58.46. Mpinzani wake wa karibu Edward habarimpya.comLowassa wa chama cha Chadema alijipatia kura 6,072,848 ikiwa ni asilimia 39.97 ya kura zote halali.

Matokeo hayo yamepingwa na Bw Lowassa na chama chake.
Akiwahutubia wanahabari kabla ya kutangazwa kwa matokeo Bw Lowassa alidai tume imeshirikiana na chama tawala kumpokonya ushindi. Aliitaka tume hiyo kumtangaza kuwa mshindi.
Lakini tume hiyo imejitetea na kusema mchakato wote ulikuwa huru na wa haki na kwamba uliendeshwa kwa kufuata katiba. Bw Magufuli, ambaye alikuwa Waziri wa Ujenzi katika serikali ya Rais Kikwete, anatarajiwa kuapishwa kuwa rais katika muda wa siku saba zijazo. chanzo BBC

Karibu sana mdau wa tovuti yetu

Ndugu wadau na wasomaji wa tovuti ya Habarimpya.com ,Kampuni ya Japo Investment Network inayomiliki mtandao wa Habarimpya.com inaomba radhi kwa mtandao huo kutokuwa hewani tangu leo asubuhi ,kutokana na sababu ambazo ziko nje ya uwezo wetu.
 Mhariri mtendaji wa tovuti ya Habarimpya.com,Jackson Odoyo akiandaa habari kabla ya kuzirusha hewani.

Ingawa wataalum wetu wa masuala ya IT wanaendelea kutatua sababu hizo, tumeamua kuwaletea tovuti nyingine ya www.Habarimpya-tz.blogspot.com.
Kupitia tovuti hii mtaendelea kupata taarifa zote za muhimu kutoka nje na ndani ya nchi, poleni sana kwa usumbufu na karibu sana.

John Magufuli CCM 8,882,935 58.46

 
Magufuli alikuwa Waziri wa Ujenzi katika serikali ya Rais Jakaya Kikwete anayeondoka mamlakani

Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha CCM John Pombe Magufuli ndiye rais mteule wa taifa la Tanzania baada ya kutangazwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili.
 
Akitoa matokeo hayo mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kuwa Magufuli, ambaye alikuwa akisherehekea siku yake ya kuzaliwa leo, alijipatia kura 8,882,935 ikiwa ni aslimia 58.46 huku mpinzani wake wa karibu Edward Lowassa wa chama cha Chadema akijipatia kura 6,072,848 ikiwa ni asilimia 39.97 ya kura zote. Dkt Magufuli alizaliwa Oktoba 29, 1959.
Haya ndiyo matokeo kamili kama yalivyotangazwa na Jaji Lubuva:
Matokeo ya uchaguzi wa urais Tanzania
Jina Chama Kura Asilimia
Anna Mghwira ACT 98,763 0.65
Chifu Yemba ADC 66,049 0.43
John Magufuli CCM 8,882,935 58.46
Edward Lowassa CHADEMA 6,072,848 39.97
Hashim Spunda CHAUMA 49,256 0.32
Janken Kasambala NRA 8,028 0.05
Macmillan Lyimo TLP 8,198 0.05
Fahmi Dovutwa UPDP 7,785 0.05

Moja kwa moja: Magufuli akabidhiwa cheti Tanzania




Msafara wa Bw Magufuli umelindwa vikali na maafisa wa usalama
11:30am: Msafara wa Rais mteule John Magufuli pamoja na ule wa Rais Jakaya Kikwete waelekea ikulu chini ya ulinzi mkali.



Anna Mghwira akimpongeza Magufuli
11:00am: Mgombea urais wa chama cha ACT Wazalendo Anna Mghwira aliyemaliza wa tatu ni miongoni mwa waliofika kumpongeza Bw Magufuli.



 
11:00am: Rais anayeondoka Jakaya Mrisho Kikwete amehudhuria hafla hiyo, sawa na kiongozi wa ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi wa Jumuiya ya Madola Rais wa zamani wa Nigeria Goodluck Jonathan. Bw Jonathan amampongeza rais mteule.



 
11:10am: John Pombe Joseph Magufuli akabidhiwa rasmi cheti cha ushindi uchaguzi wa rais uliofanyika Jumapili Oktoba 25.




 
11:00am: Hafla ya kumkabidhi Magufuli cheti inafanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.Ukumbi huo umejaa watu hadi pomoni.



 
10:20am: Jeshi la Tanzania limeonekana likisafirisha magari ya kijeshi, wanajeshi na silaha hadi visiwani Zanzibar. Matokeo ya uchaguzi visiwani humo yalifutiliwa mbali na mwenyekiti wa tume Jecha Salim Jecha.
9.00am: Mgombea urais wa chama cha CCM John Magufuli leo anakabidhiwa cheti cha ushindi na tume ya uchaguzi baada yake kutangazwa mshindi Alhamisi.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania Jaji Mstaafu Damian Lubuva alisema kuwa Magufuli, alijipatia kura 8,882,935 ikiwa ni aslimia 58.46.
Mpinzani wake wa karibu Edward Lowassa wa chama cha Chadema alijipatia kura 6,072,848 ikiwa ni asilimia 39.97 ya kura zote halali.
Baada ya kutangazwa kwa ushindi wake, wafuasi wake walisherehekea katika miji mbalimbali nchini humo. chanzo BBC Swahili

Ndugu wadau na wasomaji wa tovuti ya Habarimpya.com ,Kampuni ya Japo Investment Network inayomiliki mtandao wa Habarimpya.com inaomba radhi kwa mtandao huo kutokuwa hewani tangu leo asubuhi ,kutokana na sababu ambazo ziko nje ya uwezo wetu.

Ingawa wataalum wetu wa masuala ya IT wanaendelea kutatua sababu hizo, tumeamua kuwaletea tovuti nyingine ya www.Habarimpya-tz.blogspot.com.
Kupitia tovuti hii mtaendelea kupata taarifa zote za muhimu kutoka nje na ndani ya nchi, poleni sana kwa usumbufu na karibu sana.